Thursday, July 14, 2016

TCU WAMETANGAZA MABADILIKO YA TARATIBU,VIGEZO NA SIFA ZA KUJIUNGA CHUO KIKUU MWAKA WA MASOMO 2016/2017



































FORM SIX LAZIMA UWE NA TWO PRINCIPAL PASSES (YAANI D MBILI KATIKA COMBINATION YAKO) BADALA YA E MBILI KAMA ILIVYOKUWA AWALI*
*EQUIVALENT APPLICANTS (DIPLOMA) LAZIMA UWE NA GPA 3.5 KUENDELEA,AU WASTANI WA B KWENYE MASOMO YAKO KWA DIPLOMA YA ELIMU NA AFYA,AU UPPER SECOND CLASS FOR DIPLOMA*
*PRENTRY COURSE ZOTE KWA WANAFUNZI WALIOKUWA HAWANA SIFA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU ZIMESIMAMISHWA

SOMA VIGEZO VYOTE>>> HAPA


Thursday, July 7, 2016

UTEUZI WA WAKURUGENZI, PENDO MALABEJA ABAKIZWA KWIMBA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 07 Julai, 2016 amefanya uteuzi wa wakurugenzi wa halmashauri za majiji 5, Manispaa 21, Miji 22 na Wilaya (DC) 137 za Tanzania Bara.
Uteuzi huo umetangazwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe ambapo kati ya wakurugenzi wote 185 walioteuliwa, 65 wameteuliwa kutoka orodha ya wakurugenzi wa zamani na 120 ni wakurugenzi wapya.
Orodha ya wakurugenzi walioteuliwa kulingana na mikoa yao ni kama ifuatavyo;
ARUSHA
1.     Arusha Jiji                              -           Athumani Juma Kihamia
2.     Arusha DC                            -           Dkt. Wilson Mahera Charles
3.     Karatu DC                             -           Banda Kamwande Sonoko
4.     Longido DC                          -           Jumaa Mohamed Mhiwapijei
5.     Meru DC                               -           Kazeri Christopher Japhet
6.     Monduli DC                         -           Stephen Anderson Ulaya
7.     Ngorongoro DC                   -           Raphael John Siumbu

DAR ES SALAAM
1.     Dar es salaam Jiji                  -           Siporah Jonathan Liana
2.     Kinondoni Manispaa           -           Aron Titus Kagurumjuli
3.     Temeke Manispaa               -           Nassibu Bakari Mmbaga
4.     Ilala Manispaa                      -           Msongela Nitu Palela
5.     Kigamboni Manispaa           -           Stephen Edward Katemba
6.     Ubungo Manispaa               -           Kayombo Lipesi John
DODOMA
1.     Dodoma Manispaa              -           Dkt. Leonard M. Masale
2.     Kondoa DC                          -           Kibasa Falesy Mohamed
3.     Kondoa Mji                           -           Khalifa Kondo Mponda
4.     Mpwapwa DC                       -           Mohamed Ahamed Maje
5.     Kongwa DC                           -           Mhandisi Ngusa Laurent Izengo
6.     Chemba DC                          -           Semistatus Hussein Mashimba
7.     Chamwino DC                      -           Athuman Hamis Masasi
8.     Bahi DC                                -           Rachel Marcel Chuwa

Tuesday, July 5, 2016

Maagizo ya RC Mongella kwa wakuu wa wilaya wapya mkoa wa Mwanza


Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amewaapisha wakuu wapya wa Wilaya za Mkoa wa Mwanza na kuwapa vitendea kazi ikiwapo katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Ilani ya Chama Tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2015- 2020, kwaajili ya kwenda kutimiza wajibu wao wa kikatiba kwenye wilaya walizo pangiwa.

Akizungumza baada yakuwaapisha, Mhe. Mongella, amewataka waende wakasimamie shughuli za kuhimiza maendeleo, suala la ulinzi na usalama kwenye wilaya zao, huku akitilia mkazo ukomeshwaji wa mauwaji ya watu wenye ulemavu wa Ngozi albino pamoja na Vikongwe. Amesema, ikiwa jamii ya watu hao itapata madhara basi ni dhahiri Mkuu huyo wa Wilaya atakuwa ameshindwa kusimamia majukumu yake.

Mkuu huyo wa mkoa pia, amerudia kauli yake nakuwataka viongozi hao wapya watambue wanajukumu zito lililoko mbele yao, ikiwa ni pamoja na kukomesha Utumiaji wa dawa zakulevya.

Aidha ameonya uchezaji wa Pool na unywaji wa Pombe wakati wa saa kazi, huku akimsisitiza mkuu wa Wilaya ya Nyamagana kuhakikisha ifikapo Agosti mosi, suala la wafanyabiashara wanaofanya biashara kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi liwe limepatiwa ufumbuzi.

Mongella amesema, katika mkoa wa Mwanza, Hotel na Clabu, yeyote ile, iwe ya kawaida au ya Kitalii, ikibainika inafanya biashara ya Shisha, hawataivumilia na badala yake wataifutia Leseni ya biashara.

Walio apa mbele ya Mkuu wa Mkoa, ambao waliteuliwa na Mhe. Rais Tarehe 26, Juni, 2016 ni Emmanuel Enock Kipole, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Estomin Francis Chang’a Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Hadija Rashid Nyembo Mkuu wa Wilaya ya Magu, wengine ni Juma Samwel Sweda Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Dkt. Leonard Moses Masale Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mary Onesmo Tesha Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana na Mhandisi Mtemi Msafiri Simioni Mkuu wa Wilaya ya Kwimba.

Imetolewa na
Atley J. Kuni
Afisa habari na Mahusiano
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
MWANZA.
04, Julai, 2016.


Sunday, June 26, 2016

UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA WAPYA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425      
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.
Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.
Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.
Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.
Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
1.     Arusha           -           Mrisho Mashaka Gambo
2.     Arumeru        -           Alexander Pastory Mnyeti
3.     Ngorongoro  -           Rashid Mfaume Taka
4.     Longido         -           Daniel Geofrey Chongolo
5.     Monduli         -           Idd Hassan Kimanta
6.     Karatu                        -Therezia Jonathan Mahongo


DAR ES SALAAM
1.     Kinondoni     -           Ally Hapi
2.     Ilala                -           Sophia Mjema
3.     Temeke         -           Felix Jackson Lyaviva
4.     Kigamboni     -           Hashim Shaibu Mgandilwa
5.     Ubungo          -           Hamphrey Polepole

IDADI YA WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA 5 KWA KILA SHULE ZILIZOPO WILAYA YA KWIMBA.

June 24 2016 Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ‘TAMISEMI’ imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2016. Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali.
Jumla ya wanafunzi 65,720 wakiwemo wasichana 29,457 na wavulana 36,263wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 34,064 wakiwemo wasichana 13,466 na wavulana 20,598 sawa na asilimia 52 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati.
Wanafunzi 30,897 wakiwemo wasichana 15,445 na wavulana 15,452 sawa na asilimia 47 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara na wanafunzi 759 wakiwemo wasichana 220 na wavulana 539 sawa na asilimia 1 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.
Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2016 wataanza muhula wa kwanza July 11 2016 na hakutakuwa na mabadiliko yoyote ya shule.
Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati, endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti July 24 ambayo ndiyo siku ya mwisho ya kuripoti nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine aliyekosa nafasi

WALIOCHAGULIWA KWA SHULE ZA SEKONDARI, WILAYA YA KWIMBA KUJIUNGA KIDATO CHA 5 MWAKA 2016

BUJIKU SAKILA
·        Waliopata daraja(i-iii)-37
·        Wamechaguliwa wanafunzi 35.
NGUDU 
·        Waliopata daraja(i-iii)-24.
·        Wamechaguliwa wanafunzi 22.
NYAMILAMA
·        Waliopata daraja(i-iii)-36.
·        Wamechaguliwa wanafunzi 21.
MWAMASHIMBA
·        Waliopata daraja(i-iii)-32
·        Wamechaguliwa wanafunzi 20.
Previous Page Next Page Home