JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO
YA RAIS IKULU
Simu : +255-22-2114512, 2116898
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya
mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya
139.
Katibu Mkuu Kiongozi
Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua
aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack
anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna
Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia
amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano
Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw.
Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam
ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli
amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa
anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi
wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa
walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu
Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya
uongozi.
Wakati
huo huo, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya
uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi
Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo
kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka
60 ameamua wastaafu.
Mhe. Rais amewashukuru
sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali
itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.
Katika uteuzi huo, Wakuu
wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais
Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya
kutokana na utendaji wao mzuri.
Aidha, nafasi 78 za
uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa
mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu
katika maeneo mbalimbali.
Walioteuliwa kuwa wakuu
wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
1.
Arusha
- Mrisho Mashaka
Gambo
2.
Arumeru
- Alexander Pastory
Mnyeti
3.
Ngorongoro
- Rashid Mfaume
Taka
4.
Longido
- Daniel Geofrey
Chongolo
5.
Monduli
- Idd Hassan
Kimanta
6.
Karatu
-Therezia Jonathan
Mahongo
DAR ES SALAAM
1.
Kinondoni
- Ally Hapi
2.
Ilala
- Sophia Mjema
3.
Temeke
- Felix Jackson
Lyaviva
4.
Kigamboni
- Hashim Shaibu
Mgandilwa
5.
Ubungo
- Hamphrey Polepole