Friday, July 10, 2015

HOTUBA YA MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAGANA NA BUNGE NA KULIVUNJA BUNGE LA KUMI LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, UKUMBI WA BUNGE, DODOMA TAREHE 9 JULAI, 2015


Chanzo :ikulu

 Mheshimiwa Spika;
Tunayo kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa kutujalia uzima na kutuwezesha kuishuhudia siku hii adhimu katika historia ya Bunge letu na nchi yetu.  Hatimaye siku ya kuvunja Bunge la Kumi imewadia ili kuwezesha hatua husika za mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ziweze kutekelezwa.
Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kunipatia nafasi hii ya kulihutubia Bunge lako tukufu ili niweze kutimiza wajibu wangu huo wa msingi Kikatiba.  Lakini, shukrani zangu kubwa ni kwa uongozi wako mahiri na shupavu.  Umeliongoza Bunge vizuri.  Najua haikuwa kazi rahisi. Penye wengi pana mengi. Lakini kwa uhodari mkubwa umeweza kulifikisha jahazi bandarini salama salmini.  Hakika wewe ni nahodha makini na jemedari hodari, uliyethibitisha uhodari na umakini wako katika uwanja wa medani.  Wewe ndiwe mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huu wa juu kabisa katika mhimili huu wa kutunga sheria na umeidhihirishia dunia kuwa wanawake wakipewa nafasi wanaweza.

Thursday, July 2, 2015

Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano,wilaya ya KWIMBA 2015/ 2016


OWM-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015.Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali.

Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi.

  
Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 nawavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansina Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 nawavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomoya Sanaa na Biashara.

Friday, June 26, 2015

HOTUBA YA KAIMU KATIBU MTENDAJI WA BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE) KUHUSU TAMKO LA BARAZA LA KUVIFUTIA USAJILI BAADHI YA VYUO NA KUVISHUSHA HADHI VINGINE



Ndugu waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, ninayo furaha kubwa kuwakaribisha katika ofisi za Baraza. Lengo la kuwaita hapa leo ni kuwapa taarifa juu ya maamuzi yaliyofikiwa na Baraza ikiwa ni katika jitihada za kuinua ubora wa elimu ya ufundi nchini.

Ndugu Waandishi wa Habari

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi ni chombo kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge Sura ya 129, kwa lengo la kusimamia na kuratibu taaluma zinazotolewa na taasisi na vyuo vva elimu ya ufundi nchini, ambavyo siyo vyuo vikuu au vyuo vikuu vishiriki. Jukumu kubwa la Baraza ni kuendeleza na kuinua ubora wa elimu ya ufundi nchini kwa kusimamia kikamilifu shughuli za kuendesha mafunzo ili tuzo zinazotolewa na taasisi na vyuo ziwe na ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa.

Kwa kutumia Sheria na Kanuni za Baraza za Usajili (2001) na zile za Ithibati na Utambuzi (2001), mnamo tarehe 20 Februari 2015, Baraza lilitoa notisi ya siku 30 kwa taasisi na vyuo vilivyokiuka taratibu na vyenye mapungufu makubwa ya Usajili na Ithibati kupitia taarifa yake kwa Umma. Notisi hii ililenga kuzipa taasisi na vyuo nafasi ya kujirekebisha. 

Baraza linakiri kuwa taasisi na vyuo vingi kama vilivyoorodheshwa kwenye Jedwali Na. 1, Jedwali Na. 3, na baadhi kwenye Jedwali Na. 5 vimechukua hatua mbalimbali za kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza. Hata hivyo, hadi kufikia leo tarehe 24 Juni 2015 yaani siku 124 baada ya Notisi ya Baraza, kuna vyuo ambavyo havijachukua hatua yoyote ya kurekebisha mapungufu yake kama inavyooneshwa kwenye Jedwali Na. 2 na Jedwali Na. 4.

Tamko la Baraza

Kutokana na mapungufu hayo Baraza limeamua kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zake kwa taasisi na vyuo vyote vilivyoorodheshwa katika Jedwali Na. 2 na Jedwali Na. 4 kwa makosa yafuatayo:

a)    Ama kumalizika kwa muda wa  Usajili wa Awali (Preparatory Registration) na Usajili wa Muda (Provisional Registration); au
b)    Kutoanza mchakato wa kupata Ithibati baada ya kupata Usajili Kamili; au
c)    Kumalizika kwa muda wa Ithibati na kutochukua hatua ya kuomba upya Ithibati (re-affirmation); na
d)    Taasisi na Vyuo kuamua vyenyewe kusitisha kutoa mafunzo kwa sababu mbalimbali.

Tuesday, June 16, 2015

Friday, June 12, 2015

Makadirio ya Idadi ya Wapiga Kura kwa Wilaya ya Kwimba Mwaka 2015


Makadirio ya idadi ya watu wenye umri wa kupiga kura katika mkoa
wa Mwanza ni (1,403,743). Haya ni makadirio ya idadi ya watu ambao
watakuwa na umri wa miaka 18 na zaidi hadi kufikia uchaguzi wa
mwaka 2015.

Mkoa wa Mwanza una majimbo 9 ya uchaguzi. Jimbo la Buchosa
linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya watu wenye umri wa
kupiga kura (217,733) likifuatiwa na Jimbo la Nyamagana (210,220).
Jimbo lenye idadi ndogo zaidi ya watu wenye umri wa kupiga kura
ni Sumve ambalo lina watu 87,993.

Hapa chini imewekwa orodha ya majimbo ya wilaya ya kwimba, kata zake, makadirio ya idadi ya watu mwaka 2015 na makadirio ya idadi ya watu wenye umri wa miaka 18 na zaidi



Kusoma idadi kamili ya Makadirio ya Idadi ya Wapiga Kura kwa Mkoa, Mwaka 2015
SOMA HAPA=>>>>>> FUNGUA HAPA

Soma Bajeti ya Mwaka 2015/ 2016 Iliyowasilishwa na Waziri Wa Fedha Jana Bungeni




Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum Mkuya (MB) akiwasilisha bungeni Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/16, Mjini Dodoma jana.

 SOMA BAJETI YA MWAKA 2015/16 HAPA===>>>BAJETI YA MWAKA 2015/16

Monday, June 8, 2015

MULONGO AZINDUA MASHINDANO YA U13 TAIFA JIJINI MWANZA


Mkuu  wa mkoa wa Mwanza Mh. Magessa Mulongo jana kwenye uwanja wa CCM Kirumba akifungua mashindano ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 13

Akifungu mashindano hayo Mh Mulongo amewataka vijana hao kujituma katika michezo na masomo kwa kuwa vyote vinakwenda sambamba

Amesisitiza shirikisho la mpira Tanzania TFF kuongeza juhudi katika kuendeleza soka la vijana

Katika salamu zake za utangulizi Rais wa TFF Jamal Malinzi ameeleza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuibua timu ya vijana wenye umri wa miaka 13 ambao watahamishiwa kwenye shule ya Alliance, watakuwa hapo kusoma na kufundishwa mpira.


Mpango wa TFF ni kuwa hadi kufikia mwaka 2019 timu hii itakuwa imara kuiwakilisha Tanzania katika mashindanoya fainali za Afrika umri chini ya miaka 17, fainali ambazo zitafanyika Tanzania

Mikoa yote 25 ya Tanzania bara inashiriki mashindano haya na mkoa wa Dar es salaam umewakilishwa na timu tatu Kinindoni, Ilala na Temeke.
TFF inashukuru Symbion power kwa ushirikiano wa kuendeleza mpira wa vijana


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA(TFF)



Previous Page Next Page Home