(Makala hii ipo katika toleo la gazeti la habarileo la may 9
2015)
MICHEZO ni afya walisema wahenga
tangu enzi za mababu zetu. Nami sina budi kukubaliana na msemo wa wahenga hawa
kwani nimeshuhudia michezo ikijenga afya na kudumisha undugu ama kujenga
urafiki.
Mafanikio na maendeleo ya michezo
Tanzania ni matokeo ya muda mrefu ya juhudi za serikali kwa kushirikiana na
wadau wengine kuhakikisha taifa linapata wanamichezo wenye vipaji na
kuwaendeleza ili wafikie ndoto za kutwaa ubingwa kwenye mashindano mbalimbali
ndani na nje ya nchi.
Katika kuzungumzia mafanikio haya
ya michezo na maendeleo ya taaluma hii, makala haya yatajikita zaidi katika
kuzungumzia chuo pekee cha kuzalisha wataalamu na walimu wa michezo Tanzania,
Chuo cha Michezo cha Malya.






