Saturday, January 24, 2015

RAIS KIKWETE KAFANYA MABADILIKO KWENYE BARAZA LA MAWAZIRI



Katibu mkuu kiongozi, Balozi Ombeni sefue akizungumza na vyombo vya habari jioni hii wakati akitangaza mabadiliko madogo ya baraza la mawazili, Ikulu jijini Dar es salaam
Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete leo amefanya mabadiliko madogo katika Baraza lake la mawaziri, ambalo Ameliapisha jioni hii Ikulu jijini Dar es salaam
Hayo yamefanyika ikiwa ni baada ya aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini kujiuzulu wadhifa wake

Hawa ndiyo Mawaziri 8 walioteuliwa na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete leo
 
1.George Simbachawene- Waziri wa Nishati na Madini
2.Mary Nagu -Waziri wa nchi Mahusiano na Uratibu
3.Harrison Mwakyembe - Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
4.Wiliam Lukuvi - Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
5.Steven Wassira - Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika
6.Samwel Sitta - Waziri wa Uchukuzi
7.Jenista Mhagama - Waziri wa Sera na Uratibu wa Bunge 

8.Christopher Chiza- Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji 



Manaibu Waziri  5 walioteuliwa
1.Steven Masele - Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano
2.Angellah Kairuki - Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi
3.Ummy Mwalimu- Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
4.Anna Kilango- Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
5.Charles Mwijage - Naibu Waziri wa Nishati na Madini

No comments:

Post a Comment

Previous Page Next Page Home