Saturday, January 30, 2016

MBUNGE MANSOOR SHANIF HIRAN, JIMBO LA KWIMBA NA KWIMBA TUITAKAYO.

Mh Mansoor Shanif Hirani, Mbunge jimbo la KWIMBA(2015-2020)

By NGUDU NYUMBANI BLOG
30/01/2016.

NDUGU Mansoor Shanif Hirani alizaliwa Tar 05/05/1967, kwa maana hiyo ikifika Tarehe 05 may mwaka huu atafikisha miaka 49. Amesoma katika shule ya msingi “Nyakahoja” kuanzia 1975-1981, pia kasoma shule ya sekondari ya “Lake” kuanzia mwaka 1982-1986.

Kwa sasa ndiye Mbunge halali wa Jimbo la KWIMBA kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), pia ndiye mweka hazina wa mkoa wa Mwanza (Ccm) wadhifa aliokuwa nao tangu 2012. Pia ndiye katibu mkuu mtendaji wa kampuni la "Mansoor industries ltd". Bila kusahau kuwa ni mjumbe wa kamati za kudumu za bunge (bunge la 11) kwenye kamati ya “MIUNDOMBINU”. Anafahamika Kwa nick-name “MOIL”.

HISTORIA

“Mkoa wa mwanza ulianzishwa rasmi mwaka 1963 ukiwa na wilaya nne za Ukerewe. Geita, Mwanza na Kwimba. Mwaka 1972  baada ya sera ya madaraka mikoani wilaya zaidi  zilianzishwa kwa kuanza na Magu mwaka 1974. Wilaya ya  Sengerema ilianzishwa mwaka 1975 ambapo awali ilikuwa  ni tarafa mojawapo ya wilaya ya Geita.  Misungwi  ilianzishwa mwaka 1995 ambapo awali ilikuwa ni eneo la tarafa za wilaya ya Kwimba, Ilemela na Nyamagana  zilianzishwa mwaka 2002 ambazo zilikuwa zinaunda  wilaya ya mwanza”. [TAARIFA YA MKOA WA MWANZA WAKATI WA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA 1961-2011]


Sunday, January 24, 2016

MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE(SFNA) 2015


BY NGUDU NYUMBANI BLOG

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), limetangaza matokeo ya mitihani ya kujipima ya darasa la nne huku matokeo hayo yakionyesha wanafunzi wengi wamefeli katika somo la Kiingereza kwa asilimia 65.67 katika mitihani hiyo iliyofanyika mwishoni 2015.

Akitangaza matokeo hayo  Jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt. Charles Msonde amesema juhudi za makusudi zinahitajika katika kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzia ili kuboresha kiwango cha ufaulu.

Jumla ya wanafunzi 869,057 kati ya wanafunzi 977,886 sawa na asilimia 88.87 waliofanya upimaji wamepata alama katika madaraja ya A,B,C, na D. Wanafunzi 108,829 sawa na asilimia11.13 wamepata alama za ufaulu usioridhisha.

Aidha wanafunzi wamefanya vizuri zaidi katika somo la Sayansi kwa asilimia 89.44, na baraza limewataka walimu kuweka mkazo zaidi kwa wanafunzi waliofanya vibaya ili wawasaidie kuimarika na waweze kupata ufaulu mzuri.

MATOKEO UPANDE WA WILAYA YA KWIMBA

Kwa upande wa matokeo hayo ya upimaji wa kitaifa darasa la nne, ambapo kuna jumla ya shule za msingi 151.

Baadhi ya Shule za msingi zilizoongoza katika upimaji wa matokeo hayo ni kama ifuatavyo;

1. KINAMWELI PRIMARY SCHOOL

2. NG'WAMAKOYE PRIMARY SCHOOL

3. MWAKILYAMBITI PRIMARY SCHOOL

4. MWANG'HALANGA PRIMARY SCHOOL



Baadhi ya Shule zilizofanya vibaya katika upimaji huo ni;

149. NG'WANG'HANGA PRIMARY SCHOOL


151. NG'WAMAPALALA PRIMARY SCHOOL

Matokeo yote upande wa wilaya yetu ya Kwimba unaweza kuyapata kupitia link hii


>>>> MATOKEO

au ukiingia kwenye tovuti ya NECTA

Thursday, January 21, 2016

MCHANGANUO WA WABUNGE KATIKA KAMATI ZA BUNGE LA KUMI NA MOJA

MCHANGANUO WA WABUNGE KATIKA KAMATI ZA BUNGE LA KUMI NA MOJA




Wabunge wa majimbo ya KWIMBA na SUMVE wilaya ya KWIMBA wamepata nafasi katika kamati hizo za kudumu za bunge ambapo;

Mbunge wa Kwimba, MH Mansoor Shanif Hirani yupo kwenye kamati namba 14 ya MIUNDO MBINU

Mbunge wa SUMVE Ndugu Richard Mganga Ndasa yupo kwenye kamati  namba 20 ya “UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA”

Orodha kamili ya kamati zote 20 na wajumbe wake unaweza kuipata kupitia link hii




RIPOTI YA MWAKA 2015 JUU YA MAMBO YALIYOJIRI KWA HISANI YA NGUDU NYUMBANI BLOG


RIPOTI YA MWAKA JUU YA MAMBO YALIYOJIRI KWA HISANI YA NGUDU NYUMBANI BLOG

Hii ni ripoti iliyojumuisha mambo mbalimbali ambayo blogu ya Ngudu nyumbani (www.ngudukwimba.blogspot.com) ilipata kuyakusanya kwa mwaka huu kutoka vyanzo mbalimbali vya habari na watu binafsi. Hivyo imepata kuyapanga mambo kwenye makundi kama yalivyoainishwa hapo chini. Twende pamoja…

ULINZI NA USALAMA
Katika hili mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ambaye ni mkuu wa wilaya ambapo chombo cha ulinzi na usalama ndio washauri wake hivyo yeye ndiye mwenye jukumu kubwa la kuhakikisha anafuatilia kwa ukaribu zaidi usalama wa raia wake. Ndani ya mwaka huu kumepata kutokea matukio baadhi ambayo kwa namna moja au nyingine hayakuleta picha nzuri kwenye jamii yetu.

LETICIA MAGENI NYERERE AFARIKI DUNIA


ALIYEWAHI kuwa Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Chadema, Leticia Nyerere amefariki dunia.
Leticia alifariki dunia katika Hospitali ya Doctors Community iliyopo Lanham, Maryland jana (Tar 11 jan 2016) saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, alikokuwa amelazwa kwa matibabu.
Taarifa za awali kutoka Marekani, ambako msiba huo umetokea, ziliarifu kuwa msiba upo DMV 9004 Brightlea Court, Lanham, MD 20706.
Msemaji wa familia hiyo, Mbunge wa zamani wa Chadema, John Shibuda alithibitisha kutokea kwa msiba huo. Alisema ndugu wanajipanga kukutana na kuamua cha kufanya.
“Ndugu yangu ni kweli msiba umetokea wa mpendwa wetu Leticia Nyerere, umetokea jana mchana huko Marekani na huku kwetu ilikuwa ni usiku, hivyo ndugu bado hatujakutana na kuamua kwa pamoja ni wapi tuweke msiba na lini tutazika,” alisema Shibuda.
Shibuda alisema kuwa leo familia itatoa taarifa kamili ya taratibu zote za msiba huo baada ya wanafamilia kukutana.

MATOKEO YA KIDATO CHA PILI

MATOKEO YA KIDATO CHA PILI

Jumla ya wanafunzi 324,068 wa kidato cha pili sawa na asilimia 89.12 ya wanafunzi  363,666 waliofanya mtihani  wamefaulu kuendelea na kidato cha 3 mwaka 2016.

Jumla ya watahiniwa 164,547 sawa na asilimia 89.00 ya watahiniwa wote wa kike waliofanya mtihani huo wamefaulu.  Kwa upande wa watahiniwa wa kiume, 

watahiniwa 159,521 sawa na asilimia 89.24 ya watahiniwa wote wamefaulu mtihani.
 Huku wanafunzi 39,567 sawa na asilimia 10.88 wameshindwa kukidhi viwango vya kuwaruhusu kuendelea na kidato cha 3

Ufaulu umeshuka kwa baadhi ya masomo kama Uraia, Historia, Jiografia, Kingereza, Fizikia, Biolojia, Hisabati na Book keeping ukilinganisha na mwaka jana
Mikoa ya Mwanza, Dar es salaam, Mbeya na Iringa ndiyo imetoa shulle 10 bora, huku shule 10 zilizofanya vibaya zikitoka katika mikoa ya Tanga, Mtwara, Lindi na Dar es salaam.

MATOKEO YA NGUDU SEC NA BUJIKU SAKILA SEC

NGUDU SECONDARY SCHOOL

Shule ilikuwa na watahiniwa 103 ambao walitakiwa kufanya mtihani wa kidato cha pili ambapo mpangilio wa madaraja (class) upo kama ifuatavyo;
Distinction-4
Merit-12
Credit-18
Pass-53
Absent-6 (hawakufanya mtihani)
Referred-10 (waliorudia mwaka wa masomo)
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
Repeater-7 (hawa ni wale waliokuwa wamerudia mwaka)
WALIOONGOZA
-         JONIA JULIAS WANJARA. Ana GPA ya 3.3, Class ni MERIT (Upande wa wasichana)
-         ABDALLAH HEMED NG'OE. Ana GPA ya 5.0  Class ni DISTINCTION (Upande wa wavulana)

BUJIKU SEC SCHOOL

Shule ilikuwa na watahiniwa 143 ambao walitakiwa kufanya mtihani wa kidato cha pili ambapo mpangilio wa madaraja(class) upo kama ifuatavyo;
Distinction-16
Merit-17
Credit-30
Pass-69
Absent-8
Referred-4
--------------------------------------------------------------------------------------------
Repeaters-25
WALIOONGOZA
-         DEVOTHA JERAD LUCAS. Ana GPA ya 4.4, Class ni Distinction
-         HASSANI RAJABU HASSAN. Ana GPA ya 4.7, Class ni DISTINCTION
-         PETER LAMECK YUMBU. Ana GPA ya  4.7, Class ni DISTINCTION

Matokeo yote ya kidato cha pili unaweza kuyapata kupitia link hii http://necta.go.tz/matokeo/ftna2015/html/index.htm au tembelea tovuti ya NECTA kwa maelezo zaidi.

Ukijaribu kulinganisha matokeo ya shule hizi mbili utaona Bujiku Sakila wamefanya vizuri kuliko Ngudu sec. Hali hii imekuwa ikijitokeza hata kwenye matokeo ya kidato cha 4, kwamba Bujiku wanaendelea kuwazidi Ngudu sec katika ufaulu.

Ukichunguza zaidi unashindwa kujua sababu za kwanini shule kongwe kama Ngudu inakuwa na muendelezo wa matokeo mabaya kuanzia form 2 na form 4 ukilinganisha na shule nyingine ambazo bado hazijawa na miundombinu na rasilimali nyingi kama ilivyo kwa shule hii kongwe

Bado shule nyingi zimekuwa na changamoto nyingi hasa za mazingira mazuri ya kusomea, walimu wa kutosha, upatikanaji wa huduma za kijamii n.k. Mwishoni mwa mwaka jana tumeshuhudia walimu takribani 300(wa msingi na sekondari) wakipanga kugoma kufundisha kama madai yao hayajashughulikiwa.

Wanafunzi waliopata Merit, Credit  na Pass wana kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha wanafanya vizuri kidato cha nne vinginevyo ndiyo tutaendelea kuzalisha vijana wengi wasio na cha kufanya maeneo mengi ya wilaya yetu hasa ya stend almaarufu kama SOKO MJINGA, kusinda wakitabiri matokeo(BETTING) ili siku ziende. Na pengine wahusika wa elimu hawaoni kama kuna tatizo lolote katika mfululizo wa matokeo mabovu haya,.

Mwaka huu tunaanza sera ya ELIMU BURE kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne, japo sidhani kama inaweza kuwa bora kama kwanza changamoto za miaka mingi zinazoikumba sekta hii hazijapatiwa ufumbuzi wa kudumu.
NGUDU NYUMBANI

@2016
Previous Page Next Page Home