Sunday, November 29, 2015

TAARIFA KWA UMMA JUU YA KILIMO MKOA WA MWANZA.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA TAARIFA KWA UMMA TAREHE 18/11/2015

Ndugu Wanahabari.
Mkoa wa Mwanza kwa kawaida hupata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. Misimu hiyo ni ya mvua za vuli na masika ambapo mvua za vuli huanza kunyesha mwezi Septema/Oktoba hadi kufikia mwezi Januari; na msimu wa mvua za masika hunyesha Kuanzia mwezi Machi hadi Mei ya kila mwaka. Wastani wa mvua ni mm 720 hadi mm 1200 kwa mwaka ambazo hutawanyika kati ya mm 570 mm kwa mwaka hadi mm 1800 kwa mwaka.

Ndugu Wanahabari.
 Mkoa wa Mwanza unatarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani kwa maana ya mvua za juu ya wastani wa mm 1300 katika kipindi hicho cha Oktoba – Desemba, 2015. Hii ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
Kwa kuzingatia utabiri huo wa hali ya hewa, tunawashauri wakulima na wananchi katika Mkoa wa Mwanza kufanya yafuatayo:-
Kulima mazao ya chakula aina ya wanga yanayohitaji au kustahimili mvua za wastani hadi mvua za juu ya wastani na pia kukomaa kwa muda mfupi kiasi cha kuweza kukomaa kufikia mwezi Desemba, 2015/Januari, 2016. Mkazo zaidi utiliwe kwenye mazao ya:-
Viazi vitamu hasa mbegu (Variety) zisizolikishwa (Non-Orange Fortified) aina ya Polista na Ukerewe, “Kishiga Mdege” na matembele; pamoja na mbegu zilizolikishwa (Orange Fortified) kama Ejumla, Karotoda na Kabode.
Mazao mengine ni mahindi hasa katika ukanda wa mazao (agro-ecological zone) unaopata mvua za wastani wa mm 1100 hadi 1200 kwa mwaka au Zaidi ukanda ambao unajumuisha Tarafa za Ukara na Ilangala katika Wilaya ya Ukerewe na Tarafa za Kahunda na Buchosa katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa. Aina ya mbegu (variety) za mahindi zinazopendekezwa ni:-
(i) Aina ya mbegu ya mahindi chotara (hybrid) ni pamoja na SeedCo yenye alama ya pundamilia (SC 513), Pannar inayokomaa kwa muda mfupi (PAN 4M-19) na kati PAN 15), Delkab (DKC 8053).
 (ii) Aina ya mbegu ya mahindi isiyochotara/ya chavua huria (OPV) ni pamoja na Kilima, Stuka, TAN 600H, Kitale na TMV 1. Mpunga hususan mbegu aina ya SARO 5 (TXD 306) na Supa inayolimwa mabondeni (low land rice); na NERICA 2 na 4 zinazolimwa nchi kavu.

Ndugu Wanahabari.
Tunawashauri wananchi wetu kutenga fedha na kununua pembejeo za kilimo hasa mbegu, mbolea na dawa za kilimo mapema kwa kuzingatia kuwa matumizi ya pembejeo yanaweza kuongezeka kutokana na mvua hizo ambazo zinaweza kusababisha kuoshwa ama dawa za kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa au mfumuko wa magonjwa hasa ya ukungu kutokana na mazingira ya unyevunyevu mwingi katika ardhi na hewani. Aidha, pembejeo zinaweza kupanda bei na kuwa adimu kutokana na kutopatikana kwa wingi na kwa urahisi kwa sababu ya mvua kuharibu miundombinu ya barabara hasa katika maeneo ya vijijini na kuathiri usafirishaji mazao. Ili kupunguza gharama za uzalishaji kutokana na mvua, wakulima wanaweza kugawanya kiasi cha mbolea kinanchohitajika kwa eneo na kuweka kwa awamu lakini pia tunawashauriwa kuwatumia Maafisa Ugani katika Wilaya.

Vilevile tunawashauri wakulima kulima kwa kukinga au kuzuia mmomonyoko wa udongo kutokana na mvua hasa katika maeneo yenye miinuko na vilima. Mmomonyoko wa udongo unaweza kukingwa au kuzuiliwa kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulima kilimo cha matuta kwa kukinga/kukata mteremko, kulima na kuacha mistari (strip) ya nyasi au kufanya kilimo hifadhi. Zaidi, wakulima katika maeneo yanayo hifadhi unyevu kwa wingi au kutwaamisha maji (mabonde) wanaweza kulima kwa kufuata uelekeo wa maji kwa kuacha mistari ya nyasi kuzuia mmomonyoko wa udongo au kulima kilimo hifadhi kinachopunguza ukwatuaji wa udongo.

Ndugu wanahabari.
Tunawashauri wananchi kujiwekea akiba ya chakula hasa cha aina ya wanga kutokana na sababu kwamba mvua zinazotarajiwa katika kipindi hicho cha Oktoba na Desemba, 2015 zinaweza kuharibu miundombinu ya barabara na kusababisha ugumu wa usafirishaji wa vyakula hivyo kuleta uhaba wa vyakula katika masoko. Msisitizo wa kujiwekea akiba ya chakula unatolewa Zaidi kwa kuzingatia ukweli kwamba, Mkoa wa Mwanza wenye wakazi 2,772,509 huhitaji jumla ya Tani 708,376 za chakula aina ya wanga kwa mwaka mzima, ambapo, katika msimu wa kilimo wa 2014/2015 Mkoa ulizalisha Tani 495,863.2 za chakula aina ya wanga hivyo kuuwezesha kujitosheleza kwa 70% tu kwa chakula aina ya wanga.
Aidha, tunahimiza wafanyabishara kuleta chakula kutoka kwenye maeneo yenye ziada ya chakula aina ya wanga , lakini pia wananchi kutumia chakula kwa umakini na kuuza sehemu ya mazao ya biashara na mifugo ili kuweza kununua chakula. Aidha, Mkoa unasisitiza kuwa wafanyabiashara walioidhinishwa kununua na kuuza chakula kutoka katika maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula Sumbawanga kufanya hivyo kwani mkoa umeutengewa jumla ya Tani 5,400 za mahindi kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa nafaka katika masoko ya Mkoa wa Mwanza hii nikutokana na tathmini iliyofanywa na wadau.

Ndugu wanahabari
 Kupitia kwenu tunawaomba wananchi kujiwekea akiba ya chakula aina ya wanga katika ngazi ya kaya, kwa kuzingatia kuwa wastani wa watu katika kaya ya watu 6 katika mkoa wetu, tunawashauri kuhifadhi magunia 3 ya mahindi yenye uzito wa kilo 100 lakini pia magunia 5 ya muhogo mkavu yenye uzito wa kilo 60 kila moja sawa na kilo 314.64 katika kipindi cha Novemba 2015 na Januari 2016 endapo kaya hiyo itatumia mahindi au muhogo kama chakula cha wanga katika kipindi hicho.

 Kwa upande wa wakulima wanaotumia miundombinu ya umwagiliaji katika Skimu ya Umwagiliaji Mahiga kwenye Wilaya ya Kwimba tunawashauri kuchukua tahadhari kwani mabwawa yanaweza kukatika kutokana na mvua zinazotarajiwa na inaweza kusababisha mmomonyoko wa udongo, kusombwa mazao shambani, kukosa maji ya kumwagilia, kuongezeka kwa gharama za ukarabati wa mabwawa na hata kupoteza maisha ya watu na mali zao.

 Mwisho wakulima na wananchi kwa ujumla tunawashauri kuchukua tahadhari dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na mvua zinazotarajiwa na kuzitumia vizuri mvua hizo katika kuzalisha mazao yanayopendekezwa ili Mkoa uzalishe chakula cha kuutosheleza katika msimu wa 2016/2017. Mara baada yakusema hayo niwashukuru sana kwakuja lakini zaidi sana kuweza kuchukua taarifa hii na kutufikishia kwa umma wa watanzania kupitia vyombo vyenu vya habari.

 Mungu Awabariki Sana , Ahsanteni kwa Kunisikiliza!


Chanzo:HAPA

Thursday, November 26, 2015

Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, akifungua rasmi Bunge jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, 20 Novemba 2015

Friday 20th November 2015

Mheshimiwa Spika;
Niko hapa leo kutimiza matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 91 Ibara ndogo ya kwanza inayonitaka kulihutubia na kulifungua rasmi Bunge hili. Naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya njema, na kutuwezesha kuwepo hapa siku ya leo. Aidha nitumie fursa hii kuwakumbuka wenzetu ambao, kwa namna na nafasi mbalimbali, walishiriki katika mchakato wa uchaguzi huu na kwa bahati mbaya walipoteza maisha yao kabla ya mchakato haujakamilika. Kwa hao wote waliotangulia mbele za haki ninamuomba Mwenyezi Mungu azirehemu roho zao na awape pumziko la amani. Nitumie nafasi hii kuwapa pole ndugu na jamaa ambao ndugu zao walifariki na wengine kupata ulemavu wakati wa mchakato wa uchaguzi huu.

Wednesday, November 25, 2015

HAWA NDIO WABUNGE 256 WALIOTHIBITISHWA NA TUME YA NEC


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli tayari ameapishwa na kuanza kazi… kwa upande wa Wabunge wenyewe bado.
Kinachosubiriwa ni kuitishwa kwa Bunge la 11 ambapo Spika Mteule pamoja na Wabunge wote wataapishwa… kingine kitakachofanyika ni uthibitisho wa jina la Waziri Mkuu, uchaguzi wa Naibu Spika na ufunguzi rasmi wa Bunge la 11.

Kulikuwa na stori nyingi sana wakati wa mchakato mzima wa Uchaguzi Mkuu ikiwemo matokeo kukataliwa na baadhi ya Wagombea, kwingine Uchaguzi haukufanyika kabisa, kwingine uchaguzi ulisogezwa mbele kwa sababu mbalimbali. Lakini mpaka leo November 12 2015 hapa ninayo majina ya Wabunge 256 ambayoTume ya Uchaguzi NEC imeyathibitisha kwamba wamepita kwenye Uchaguzi.

ILIKUWA NI LAZIMA MH MANSOOR ASHINDE UBUNGE JIMBO LA KWIMBA 2015


KOMANYA, BONIPHACE, mwandishi wa makala na mmiliki wa blogu
BY NGUDU NYUMBANI BLOG

Ni ukweli usiopingika kuwa, jimbo la Kwimba tangu mfumo wa vyama vingi kuasisiwa mwaka 1992,  na uchaguzi wa kwanza ukihusisha mfumo huo limeongozwa na chama tawala(CCM) kuanzia ngazi za serikali za mitaa, wawakilishi kama madiwani, mbunge, pia halmashauli kuwa chini ya usimamizi wa Ccm. Hali hiyo imeendelea kuonekana katika chaguzi zote zilizofuata nikimaanisha 2000,2005,2010 na 2015.
Japo kwenye uchaguzi wa wawakilishi serikali za mtaa mwishoni mwa mwaka jana wapinzani walipata uwakilishi kwenye baadhi ya vijiji na vitongoji japo haikubadili upepo kisiasa katika jimbo hili.

Kuna baadhi ya mambo au sababu zinazonipelekea kusema ndugu Mansoor alikuwa na nafasi kubwa kushinda ubunge jimbo la kwimba. Machache kati ya mengi ni kama ifuatavyo..

Moja, kukubalika sana maeneo mengi hasa vijijini. Hii ni kete kubwa kwa mgombea yeyote kuweka mazingira ya kushinda uchaguzi hasa ukizingatia vijijini ndio kuna mwitikio mkubwa wa wapiga kura. Imani hiyo kaijenga tangu agombee awamu iliyopita. Pia wananchi wengi walipata kumwamini katika miaka mitano iliyopita, kwa maana hiyo imani yao kubwa ilimjenga na kumpa imani kubwa ya kushinda awamu nyingine. Hapa namaanisha muitikio wao hasa kwenye kampeni zake.

Pili, nguvu ya pesa aliyonayo. Pia katika hili mgombea huyu alikuwa vizuri ukilinganisha na wapinzani wake. Katumia njia hii kucheza na akili za wananchi kwa kugawa kiasi cha fedha, nguo na vifaa vya chama. Pia katika hatua nyingine kupitia wapambe wake amegawa majembe baadhi ya vijiji kuhamasisha maendeleo. Njia hii imeongeza imani kwa wana ccm na wananchi wasio na vyama hata baadhi ya wapinzani wasio na msimamo kuwa na matumaini nae. Japo uhalisia ni kwamba inakosekana elimu ya uraia kwa wananchi kujua zawadi hizi kipindi cha kampeni hazina manufaa ya kudumu katika maisha yao ya kila siku ukizingatia hutolewa mara moja kila baada ya miaka mitano.

Tatu, kukosekana kwa upinzani imara wenye kuweza kujenga hoja na kuja na sera za kuweza kuwashawishi wananchi wawachague. Katika hili pia UKAWA kushindwa kufikia makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja na badala yake kusimamisha wawili ndugu Mh shilogela(CDM) na Mh Ntiga Otto(CUF) kulisaidia kwa kiasi kikubwa kugawana kura za upinzani na kumpa nafasi Mh mansoor kuwaacha kwa mbali kwenye mchuano.

Nne, kuwaaminisha wananchi baadhi ya mambo kama kayafanikisha. Kati hili ndugu Mansoor aliweza kuanisha mafanikio katika awamu iliyopita kama kuwaletea wananchi maji kutoka ziwa Victoria, umeme, kuwezesha ujengwaji wa  zahanati/vituo vya afya kadhaa. Kuweka mambo sawa ni kuwa kazi ya mbunge kwa mujibu wa katiba ni kuwakilisha wananchi, kutunga sheria na kusimamia serikali katika masuala ya maendeleo kama kusimamia miradi. Ila sio kweli kwamba kawaletea wananchi maji wala umeme, bali ni kupitia kuishauri na kuikumbusha serikali kufanya hayo na mengine jimboni kwake ila hana uwezo wa kutoa hela yake kufanikisha hayo. Katika hili la maji limekuwa likipigiwa kelele tangu kale na limekuwa likihubiliwa kwenye ilani ya ccm kila uchaguzi na limekuja kufanikishwa kwa kucheleweshwa kwenye uongozi wa JK japo lilikuwepo tangu enzi za Mkapa. Hapa naweza kuwapongeza Mh mansoor na Mh Leticia Nyerere ambao walipata kuliulizia utekelezaji wake kila walipopata nafasi kwenye bunge kuuliza swali au kujenga hoja kila mmoja katika nafasi yake. Katika hayo alifanikiwa kujipatia kura za kutosha.

Tano, jimbo bado ni ngome kuu(stronghood) ya chama tawala. Hili pia linachangia kwa asilimia kubwa kama sehemu ni ngome ya chama fulani miaka nenda rudi ni rahisi kwa chama husika kushinda japo kuna baadhi ya maeneo hali ilibadilika na ambaye hakutarajiwa kushinda.
Jimbo la Kwimba lipo chini ya Ccm kabla ya mfumo wa vyama vingi, baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi hadi leo huku wakijikusanyia madiwani wengi na kuweza kuisimamia halmashauri. Kwahiyo upinzani walipaswa kutumia nguvu zaidi na njia mbadala za kuwawezesha kushinda.

MAONI YANGU
Nilipata kufatilia uchaguzi kwa kuwasikiliza wagombea kama Mh Mansoor, Mh shilogela na Ndugu Ntiga kusikiliza sera zao na hoja zao juu ya uwakilishi wa jimbo letu.
 Kiukweli nilimwelewa sana ndugu Ntiga Otto jinsi alivyokuwa akiwasilisha Mipango na mikakati yake juu ya kuiongoza Kwimba, japo ni hali isiyofichika kwamba ndiye alikuwa na wasikilizaji/wananchi wachache zaidi ukilinganisha na hao wenzake wawili waliokuwa na watu wengi.
 Hawa Iswalala(UDP) na mch. Yohana(ACT) sikupata kuwasikia ama kuhudhulia kampeni zao. Bila shaka kilichomwangusha huyu kijana aliyejimbanua(Otto) ni kutokukubaliana kwenye umoja wao. Pia ‘mind set’ za wananchi wengi ambao hawako tayari kusikiliza sera na kubakia kushabikia vyama zaidi.
Salamu zangu hizi zimfikie popote alipo na asikate tama ajipange kwa awamu ijayo.
Uchaguzi umeisha, mbunge na madiwani wamepatikana, cha msingi ni kuwapa support tuweze kufikia lengo la kupiga hatua ya maendeleo jimbo na wilaya yetu kwa ujumla.
 Malalamiko ya kwamba huyu mhindi, sijui sio mzawa hayatosaidia kitu zaidi ya kushirikiana na kiongozi aliyeshinda kusukuma gurudumu la maendeleo. Pia ideology ya kuwa mbunge ndio mtu sahihi wa kuleta maendeleo jimboni, ni ya kupuuzwa tu. kila mmoja wetu anayo nafasi ya kuleta maendeleo kwenye jamii yake na sio kusubiri fulani akuletee maendeleo mlangoni.
tunawa support viongozi wa ngazi zote tukiweka itikadi za vyama vyetu pembeni. Sote ni wamoja ubaguzi ni kuonesha udhaifu.

kutokana na machache niliyoyagusia hapo juu, nashawishika kusema kwamba Ilikuwa ni lazima kwa mh. Mansoor kushinda ubunge kwenye jimbo la Kwimba mwaka 2015.

KWIMBA TUITAKAYO
nguduone@gmail.com




Friday, November 13, 2015

TUME YATOA MAELEZO NA IDADI YA MADIWANI VITI MAALUM


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UTEUZI WA MADIWANI WANAWAKE WA VITI MAALUM

Kwa mujibu wa Kifungu cha 86 A (8) cha Sheria ya Uchaguzi Serikali za Mitaa Sura ya 292, (Uchaguzi wa Madiwani) kikisomwa kwa pamoja na Vifungu vya 35 (1) (c) na 19 (1) (c) vya Sheria za Serikali za Mitaa (Tawala za Wilaya) na Na. 7 ya mwaka 1982 na Serikali za Mitaa (Tawala za Miji) Na. 8 ya mwaka 1982, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imepewa mamlaka ya kushughulikia na kutangaza Viti Maalum vya Madiwani Wanawake visivyopungua 1/3 ya Madiwani wa kuchaguliwa katika kila Halmashauri. Kwa kuwa Kata 3,957 zilifanya Uchaguzi Mkuu 2015 hivyo 1/3 yaViti Maalum vya Madiwani Wanawake ni 1,406. Hata hivyo, Tume haikuweza kugawa Viti vyote katika Halmashauri kutokana na kuahirishwa kwa Uchaguzi wa baadhi ya Kata katika baadhi ya Halmashauri nchini. Mgawanyo wa viti vilivyobaki utafanyika mara baada ya chaguzi zilizoahirishwa kufanyika.
Vyama vya Siasa vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu kwa upande wa Madiwani na kukidhi vigezo vya kisheria vya kupata Viti Maalum ni kama ifuatavyo:-


Jumla ya Viti vilivyogawanywa ni 1,392.
 Viti 14 vilivyosalia vitagawanywa mara baada ya Kata zilizoahirishiwa Uchaguzi kukamilisha zoezi la kupiga Kura
Majina ya Madiwani Wanawake wa Viti Maalum kwa kila Halmashauri walioteuliwa yataweza kupatikana kutoka Vyama na kwenye Halmashauri husika. Aidha tarehe 14/11/2015, Tume ya Taifa ya Uchaguzi itatangaza majina ya Madiwani wa Viti Maalum walioteuliwa. Ikumbukwe kuwa Tume imefanya uteuzi kwa kuzingatia Orodha iliyowasilishwa Tume na kila Chama kwa kuzingatia vipaumbele vya Chama husika.

Imetolewa na:
Jaji (Mst.) Damian Z. Lubuva
MWENYEKITI TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

12/11/2015

Friday, July 10, 2015

HOTUBA YA MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAGANA NA BUNGE NA KULIVUNJA BUNGE LA KUMI LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, UKUMBI WA BUNGE, DODOMA TAREHE 9 JULAI, 2015


Chanzo :ikulu

 Mheshimiwa Spika;
Tunayo kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa kutujalia uzima na kutuwezesha kuishuhudia siku hii adhimu katika historia ya Bunge letu na nchi yetu.  Hatimaye siku ya kuvunja Bunge la Kumi imewadia ili kuwezesha hatua husika za mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ziweze kutekelezwa.
Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kunipatia nafasi hii ya kulihutubia Bunge lako tukufu ili niweze kutimiza wajibu wangu huo wa msingi Kikatiba.  Lakini, shukrani zangu kubwa ni kwa uongozi wako mahiri na shupavu.  Umeliongoza Bunge vizuri.  Najua haikuwa kazi rahisi. Penye wengi pana mengi. Lakini kwa uhodari mkubwa umeweza kulifikisha jahazi bandarini salama salmini.  Hakika wewe ni nahodha makini na jemedari hodari, uliyethibitisha uhodari na umakini wako katika uwanja wa medani.  Wewe ndiwe mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huu wa juu kabisa katika mhimili huu wa kutunga sheria na umeidhihirishia dunia kuwa wanawake wakipewa nafasi wanaweza.

Thursday, July 2, 2015

Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano,wilaya ya KWIMBA 2015/ 2016


OWM-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015.Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali.

Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi.

  
Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 nawavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansina Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 nawavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomoya Sanaa na Biashara.

Friday, June 26, 2015

HOTUBA YA KAIMU KATIBU MTENDAJI WA BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE) KUHUSU TAMKO LA BARAZA LA KUVIFUTIA USAJILI BAADHI YA VYUO NA KUVISHUSHA HADHI VINGINE



Ndugu waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, ninayo furaha kubwa kuwakaribisha katika ofisi za Baraza. Lengo la kuwaita hapa leo ni kuwapa taarifa juu ya maamuzi yaliyofikiwa na Baraza ikiwa ni katika jitihada za kuinua ubora wa elimu ya ufundi nchini.

Ndugu Waandishi wa Habari

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi ni chombo kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge Sura ya 129, kwa lengo la kusimamia na kuratibu taaluma zinazotolewa na taasisi na vyuo vva elimu ya ufundi nchini, ambavyo siyo vyuo vikuu au vyuo vikuu vishiriki. Jukumu kubwa la Baraza ni kuendeleza na kuinua ubora wa elimu ya ufundi nchini kwa kusimamia kikamilifu shughuli za kuendesha mafunzo ili tuzo zinazotolewa na taasisi na vyuo ziwe na ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa.

Kwa kutumia Sheria na Kanuni za Baraza za Usajili (2001) na zile za Ithibati na Utambuzi (2001), mnamo tarehe 20 Februari 2015, Baraza lilitoa notisi ya siku 30 kwa taasisi na vyuo vilivyokiuka taratibu na vyenye mapungufu makubwa ya Usajili na Ithibati kupitia taarifa yake kwa Umma. Notisi hii ililenga kuzipa taasisi na vyuo nafasi ya kujirekebisha. 

Baraza linakiri kuwa taasisi na vyuo vingi kama vilivyoorodheshwa kwenye Jedwali Na. 1, Jedwali Na. 3, na baadhi kwenye Jedwali Na. 5 vimechukua hatua mbalimbali za kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza. Hata hivyo, hadi kufikia leo tarehe 24 Juni 2015 yaani siku 124 baada ya Notisi ya Baraza, kuna vyuo ambavyo havijachukua hatua yoyote ya kurekebisha mapungufu yake kama inavyooneshwa kwenye Jedwali Na. 2 na Jedwali Na. 4.

Tamko la Baraza

Kutokana na mapungufu hayo Baraza limeamua kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zake kwa taasisi na vyuo vyote vilivyoorodheshwa katika Jedwali Na. 2 na Jedwali Na. 4 kwa makosa yafuatayo:

a)    Ama kumalizika kwa muda wa  Usajili wa Awali (Preparatory Registration) na Usajili wa Muda (Provisional Registration); au
b)    Kutoanza mchakato wa kupata Ithibati baada ya kupata Usajili Kamili; au
c)    Kumalizika kwa muda wa Ithibati na kutochukua hatua ya kuomba upya Ithibati (re-affirmation); na
d)    Taasisi na Vyuo kuamua vyenyewe kusitisha kutoa mafunzo kwa sababu mbalimbali.

Tuesday, June 16, 2015

Friday, June 12, 2015

Makadirio ya Idadi ya Wapiga Kura kwa Wilaya ya Kwimba Mwaka 2015


Makadirio ya idadi ya watu wenye umri wa kupiga kura katika mkoa
wa Mwanza ni (1,403,743). Haya ni makadirio ya idadi ya watu ambao
watakuwa na umri wa miaka 18 na zaidi hadi kufikia uchaguzi wa
mwaka 2015.

Mkoa wa Mwanza una majimbo 9 ya uchaguzi. Jimbo la Buchosa
linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya watu wenye umri wa
kupiga kura (217,733) likifuatiwa na Jimbo la Nyamagana (210,220).
Jimbo lenye idadi ndogo zaidi ya watu wenye umri wa kupiga kura
ni Sumve ambalo lina watu 87,993.

Hapa chini imewekwa orodha ya majimbo ya wilaya ya kwimba, kata zake, makadirio ya idadi ya watu mwaka 2015 na makadirio ya idadi ya watu wenye umri wa miaka 18 na zaidi



Kusoma idadi kamili ya Makadirio ya Idadi ya Wapiga Kura kwa Mkoa, Mwaka 2015
SOMA HAPA=>>>>>> FUNGUA HAPA

Soma Bajeti ya Mwaka 2015/ 2016 Iliyowasilishwa na Waziri Wa Fedha Jana Bungeni




Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum Mkuya (MB) akiwasilisha bungeni Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/16, Mjini Dodoma jana.

 SOMA BAJETI YA MWAKA 2015/16 HAPA===>>>BAJETI YA MWAKA 2015/16

Monday, June 8, 2015

MULONGO AZINDUA MASHINDANO YA U13 TAIFA JIJINI MWANZA


Mkuu  wa mkoa wa Mwanza Mh. Magessa Mulongo jana kwenye uwanja wa CCM Kirumba akifungua mashindano ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 13

Akifungu mashindano hayo Mh Mulongo amewataka vijana hao kujituma katika michezo na masomo kwa kuwa vyote vinakwenda sambamba

Amesisitiza shirikisho la mpira Tanzania TFF kuongeza juhudi katika kuendeleza soka la vijana

Katika salamu zake za utangulizi Rais wa TFF Jamal Malinzi ameeleza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuibua timu ya vijana wenye umri wa miaka 13 ambao watahamishiwa kwenye shule ya Alliance, watakuwa hapo kusoma na kufundishwa mpira.


Mpango wa TFF ni kuwa hadi kufikia mwaka 2019 timu hii itakuwa imara kuiwakilisha Tanzania katika mashindanoya fainali za Afrika umri chini ya miaka 17, fainali ambazo zitafanyika Tanzania

Mikoa yote 25 ya Tanzania bara inashiriki mashindano haya na mkoa wa Dar es salaam umewakilishwa na timu tatu Kinindoni, Ilala na Temeke.
TFF inashukuru Symbion power kwa ushirikiano wa kuendeleza mpira wa vijana


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA(TFF)



MWANZA : Takukuru yawaburuza kortini vigogo watatu wa Serikali


TAASISI ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa nchini (TAKUKURU) imewaburuza mahakamani vigogo watatu  wa Serikali  kwa makosa mawili ya matumizi mabaya ya madaraka na   kutumia nyaraka mbalimbali kumtapeli mwajiri wao.

Vigogo hao ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Mkoa wa Shinyanga, Patrick Karangwa (45), Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza, Ntinika Paul (51) na Mhasibu Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mathayo Masuka.

Walifikishwa wiki iliyopita katika Mahakama ya Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza,  mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Janeth Masesa.

Ilidaiwa kuwa watuhumiwa hao walitenda makosa hayo mwaka 2009 wakati wakiwa wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Ilielezwa kuwa wakati wakitenda makosa hayo, Karangwa alikuwa Mchumi Mkuu Jiji la Mwanza, Paul   alikuwa mweka hazina mkuu  wa jiji hilo wakati  Masuka alikuwa mkaguzi wa ndani wa jiji la Mwanza.

Watuhumiwa hao walikana mashtaka hayo na wapo nje kwa dhamana na  kesi hiyo inatarajiwa kutajwa tena Juni 11 mwaka huu.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Mwanza, Kasomambuto Mbengwa, alithibitisha taasisi hiyo kuwakifikisha vigogo hao mahakamni.




Sunday, May 24, 2015

Ajira Mpya Kwa Walimu 2015........Haya Ni Majina Ya Awamu Ya Pili Pamoja Na Mabadiliko Ya Vituo Vya Kazi


Tarehe 27  na 30  Aprili, 2015,  Ofisi ya Waziri Mkuu  -  TAMISEMI ilitangaza ajira ya wahitimu wa mafunzo ya ualimu na mafundi sanifu  wa maabara  kwa  kuweka  orodha kwenye tovuti ya    www.pmoralg.go.tz.  Iliagizwa kuwa  waajiriwa    wapya walipaswa kuripoti katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kuanzia tarehe 01 hadi 09 Mei, 2015.

Napenda  kuchukua nafasi hii kuutaarifu umma  kuwa ofisi yangu  ilipokea  na kuchambua  maombi ya  walimu ambao hawakuajiriwa awali;  na walioomba kubadilishiwa vituo kutokana na    matatizo mbalimbali.

 Vilevile ofisi  imezingatia kuwapanga tena  walimu ambao kwa sababu  za msingi  walishindwa kuripoti kufikia tarehe 09 Mei, 2015.  

Walimu wote waliopo katika orodha ya awamu ya pili wanapaswa kuripoti kuanzia tarehe  01 hadi 05 Juni, 2015  kwenye ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri kwa ajili ya kuajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi.

Orodha ya walimu  hao watakaoajiriwa katika halmashauri husika  imegawanywa katika makundi yafuatayo:-

i.  walimu wa cheti (Daraja IIIA) waliokosa ajira kwa awamu ya kwanza;

ii.  walimu wa cheti (Daraja IIIA) waliobadilishiwa vituo;
iii.  walimu  wa  masomo ya sanaa  kwa ajili ya shule za sekondari  ambao hawakupangiwa vituo; 

iv.  walimu waliobadilishiwa vituo wa masomo ya sanaa  kwa ajili ya shule za sekondari; 

v.  walimu wa masomo ya sayansi na hisabati kwa ajili ya shule za sekondari ambao hawakupangiwa vituo; na

vi.  walimu  waliobadilishiwa vituo wa masomo ya sayansi na hisabati kwa ajili ya
shule za sekondari.

Utaratibu wa Ajira ya Walimu Awamu ya Pili
Kila mwajiriwa mpya anatakiwa kuzingatia yafuatayo:-i.  kuwasilisha vyeti halisi vya taaluma ya kuhitimu mafunzo  ya ualimu, elimu ya sekondari, cheti cha kuzaliwa pamoja na nakala zake; na

ii.  atalipwa  posho ya kujikimu kwa muda wa siku saba (7) na nauli ya usafiri wa magari (ground travel), malipo hayo yatatolewa na halmashauri husika.

Angalizo
i.  Walimu ambao wamekwisharipoti na mchakato wao wa ajira umeanza katika  Mamlaka za Serikali za Mitaa hawatahusika na mabadiliko  haya  hivyo waendelee kufanya kazi katika halmashauri husika na hawahusiki na upangaji wa awamu hii.

ii.  Walimu ambao walichelewa kuripoti tarehe 9 Mei, 2015 na majina yao hayajaonekana katika mabadiliko haya wanatakiwa waende kuajiriwa katika halmashauri walizopangwa awali (kwa kuzingatia orodha iliyotolewa kwenye tovuti tarehe 30/4/2015).  Aidha, walimu wa masomo ya sanaa ambao hawakuripoti katika Halmashauri za Wilaya za Meru na Arusha wamebadilishwa vituo.

iii.  Walimu waliopangwa ni wale wa masomo  ya sanaa/biashara na cheti waliohitimu mafunzo kwa mwaka wa masomo 2013/14 na wahitimu  wa miaka ya nyuma wa masomo ya sayansi na hisabati kwa ajili ya kufundisha katika shule za sekondari.

iv.  Kituo cha kazi cha mwalimu ni shule na sio Makao Makuu ya Halmashauri, posho italipwa baada ya mwalimu kuripoti na kuandika  barua kupitia kwa
Mkuu wa Shule.

v.  Mwalimu hatapokelewa na kuaajiriwa kama ikitokea yupo katika orodha na amehitimu shahada au stashahada zisizo za ualimu na wenye shahada za ualimu zisizo na somo au masomo ya kufundishia katika shule za sekondari.

vi.  Ikibainika kuna mwalimu atakayekwenda kuripoti na kuchukua posho na kuondoka, atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria.

Ni muhimu kuzingatia maelekezo haya, ikiwa ni pamoja na muda uliowekwa kuripoti kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza.

Limetolewa na
Ndg. Jumanne A. Sagini
KATIBU MKUU
OFISI YA WAZIRI MKUU-TAMISEMI 
______________










Thursday, May 21, 2015

ZIARA YA MBUNGE WA JIMBO LA KWIMBA KWA WANANCHI WAKE

Mbunge wa Kwimba Mansoor amepata mapokezi makubwa jimboni kwake.



Akiwa ameambatana na Katibu wa mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu, Mbunge huyo amekabidhi kadi 1600, mifuko ya saruji 600 yenye thamani ya shilingi milioni 12 na kuviwezesha vikundi mbalimbali zaidi ya shilingi milioni 5.

wanachama wapya

















MBUNGE MANSOOR, JIMBO LA KWIMBA LIMEBADILIKA NA KUPIGA HATUA YA 
MAENDELEO KWA VITENDO.

MBUNGE wa Jimbo la Kwimba, Shanif Mansoor,ametamba kuwa wananchi wa jimboni humo wajivune kwa kushirikiana nae kuleta maendeleo kwa vitendo na kulibadilisha badala ya kusikiliza uzushi wa baadhi ya wapinzani wake kisiasa wanaoendekeza ukabila.

Pia amekuwa akichangia miradi ya maendeleo ambapo metoa kiasi cha shilingi milioni 17 za kutekeleza ahadi zake za maendeleo na Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa vitendo katika Jimbo lake.

Mansoor alikabidhi saruji mifuko 600 katika Kata za Mhande, Fukalo, Ngudu na Bupamwa kwa ajili ya kusaidia ujenzi kwenye shule za msingi, zahanati na sekondari pamoja na kuchangia fedha na vifaa vya Kompyuta kwenye baadhi ya sekondari    na Chuo cha Afya cha Ngudu mjini.

Mbunge Mansoor akizungumza na mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara juzi uliofanyika katika viwanja vya stendi mjini Ngudu, alisema kwamba saruji hiyo aliyoitoa katika Kata ya Bupamwa kwenye vijiji vya Dodoma, Kiliwi na itegamatwi kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi.

Katika Kata ya Fukalo alitoa saruji katika vijiji vya Sanga, Msongwa, Chibuji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za msingi, Kata ya Mhande ni kijiji cha Gurumwa kwa ajili ya kusaidia pia ujenzi wa shule ya msingi na milioni tatu kwa maabara ya sekondari na Kata ya Ngudu mjini alitoa fedha kiasi cha shilingi milioni mbili sekondari ya Bujiku Sakila na shilingi milioni moja Ngudu mjini.

Maeneo mengine aliyochangia ni Chuo cha Afya Ngudu mjini shilingi milioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa choo na kutoa Komputa tatu(sh. 1.8 mil), kuchangia saruji mifuko 50 kanisa la Romani (RC) na mifuko 50 kanisa la Afrika Iniland Charch Tanzania (AICT) katika kijiji cha Kilyaboya na kikundi cha ujasilimali Ngudu mjini kilipata shilingi laki tano.

Mansoor aliwaeleza wananchi kuwa katika fedha hizo za kuchangia maendeleo hazihusiani na Mfuko wa Jimbo la Kwimba bali kutokana na nguvu yake kwa lengo la kuwasaidia wananchi ili kupiga hatua ya maendeleo, ambapo al katika Kata ya Ngudu mjini alichangia saruji pia vijiji vya Gudula (shule) na Chamela (jengo la Kiliniki).

“Thamani ya saruji ambayo leo nimeitoa kusaidia wananchi katika vijiji hivyo ni shilingi milioni 12 na jumla ya fedha zilizokabidhiwa ni shilingi milioni tano tasilimu hivyo hapa misaada yote imegharimu kiasi shilingi milioni 17 jambo ambalo ni la kujivunia kwa wananchi kwa kuwa na Mbunge anayetambua maendeleo,”alisema.

Mansoor alitamba kuwa kwa kipindi chake cha uwakilishi kwa wananchi amefanya mambo makubwa kusimamia ikiwemo, usambazaji umeme vijijini katika Kata, kupigania maji safi kutoka chanzo cha Ziwa Victoria cha Ihelele, Shinyanga- Kahama ambayo huduma imefika na barabara ya Hungumalwa, Ngudu-Magu kwa kiwango cha lami ambayo tayari upembuzi yakinifu utaanza hivi karibuni.

Mbunge    huyo alitoa wito kwa wananchi wa Jimbo la Kwimba kumpatia ushirikiano kutekeleza yale aliyoahidi kwao na kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo na kuwapuuza baadhi ya wanasiasa wachache walioanza kupitapita huku wakimchafua na kuanza kuhamasisha ukabila jambo ambalo alisema wananchi wanapashwa kutafakari na kuwataka wapinzani wake waeleze sela na hoja zitakazowashawishi kuwachagua.

chanzo: gsengo blog.


Previous Page Next Page Home