Sunday, June 26, 2016

UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA WAPYA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425      
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.
Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.
Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.
Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.
Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
1.     Arusha           -           Mrisho Mashaka Gambo
2.     Arumeru        -           Alexander Pastory Mnyeti
3.     Ngorongoro  -           Rashid Mfaume Taka
4.     Longido         -           Daniel Geofrey Chongolo
5.     Monduli         -           Idd Hassan Kimanta
6.     Karatu                        -Therezia Jonathan Mahongo


DAR ES SALAAM
1.     Kinondoni     -           Ally Hapi
2.     Ilala                -           Sophia Mjema
3.     Temeke         -           Felix Jackson Lyaviva
4.     Kigamboni     -           Hashim Shaibu Mgandilwa
5.     Ubungo          -           Hamphrey Polepole

IDADI YA WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA 5 KWA KILA SHULE ZILIZOPO WILAYA YA KWIMBA.

June 24 2016 Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ‘TAMISEMI’ imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2016. Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali.
Jumla ya wanafunzi 65,720 wakiwemo wasichana 29,457 na wavulana 36,263wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 34,064 wakiwemo wasichana 13,466 na wavulana 20,598 sawa na asilimia 52 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati.
Wanafunzi 30,897 wakiwemo wasichana 15,445 na wavulana 15,452 sawa na asilimia 47 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara na wanafunzi 759 wakiwemo wasichana 220 na wavulana 539 sawa na asilimia 1 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.
Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2016 wataanza muhula wa kwanza July 11 2016 na hakutakuwa na mabadiliko yoyote ya shule.
Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati, endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti July 24 ambayo ndiyo siku ya mwisho ya kuripoti nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine aliyekosa nafasi

WALIOCHAGULIWA KWA SHULE ZA SEKONDARI, WILAYA YA KWIMBA KUJIUNGA KIDATO CHA 5 MWAKA 2016

BUJIKU SAKILA
·        Waliopata daraja(i-iii)-37
·        Wamechaguliwa wanafunzi 35.
NGUDU 
·        Waliopata daraja(i-iii)-24.
·        Wamechaguliwa wanafunzi 22.
NYAMILAMA
·        Waliopata daraja(i-iii)-36.
·        Wamechaguliwa wanafunzi 21.
MWAMASHIMBA
·        Waliopata daraja(i-iii)-32
·        Wamechaguliwa wanafunzi 20.

Saturday, June 25, 2016

Mwanza uncovers more ghost workers


SOURCE: DAILY NEWS, 25 JUNE 2016.

MWANZA Region, in its second verification exercise on ghost workers, has discovered a total of 1,057 more such workers who did not show up during the verification process which was held from April 18 to June 3, this year.
In the first phase of the verification exercise the region led nationwide by having a total of 334 ghost workers. Mwanza Regional Commissioner (RC), Mr John Mongela, said this here yesterday when he was speaking to both the regional Secretariat and District Council civil servants.
“In order to implement President John Magufuli’s order of removing ghost workers from all payrolls, I created two teams which were led by Assistant Administrative Secretaries. “The effort also involved senior officials from my office,” he explained.
He said the teams discovered 28,068 workers who were paid salaries in February, this year, in both the regional secretariat and council. A total of 27,416 are from councils and 652 from the regional secretariat.
“The council’s workers who showed up during the verification exercise totalled 26,359 and those who did not attend were 1,057.
These are the ones whom we consider to be ghost workers,” he said. He said the region had made a detailed physical analysis of employees who did not come during the verification exercise at the council level and found that 367 out of 1,057 workers who did not attend were paid a total of 2,162, 730, 686/-.
He said among those workers 214 were absent during the same period of verification and did not work. But they were paid salaries amounting to 1,597,479, 435/- . “The teams also found out that there were 74 workers who were retired but were paid 226,677,112/-.
Some civil servants had resigned but were paid 54,383, 254/-,” he said. He added: “But the teams also found the presence of three workers who were fired. Two of them had their salary payments missing but one was paid 332,100/-.”
He said, however, that the team found the existence of two public servants who contested in the 2015 general elections were paid a total amount of 12,102, 000/-.
“But the saddest scenario involved the existence of 33 deceased servants who were paid 64,515,879/-. Now I do not know if the money (salaries) has followed them into their graves,” he quipped.
He also said that the verification exercise of ghost workers has revealed the presence of 31 public servants who were not known to their employers but were paid salaries. “This is funny, how possible is it for an employer to pay a salary to an unknown worker?
For example, in Ukerewe District Council there are public servants who are in the payroll but are not known to their employer,” he said.
He added that the region has revealed a total of 689 civil servants who did not attend the verification exercise, but they deserve to be paid their salaries due to various reasons.
He said 416 servants were transferred to other work stations, 29 were in studies, 18 were sick, 18 others were not having specific reasons and five were on vacation. In the regional secretariat, he said, 35 workers were assessed.
One had died but his bank account had received a total of 3,980,000/-. He said one servant was dismissed, but his account got a total of 3,617,820/- and one worker who resigned had 3,556,860/- deposited in his bank account.


ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI KWA MWAKA 2016


















Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Na Vyuo Vya Ufundi Kwa Mwaka 2016


SHULE ATOKAYO: NGUDU SECONDARY


                                         

Saturday, June 18, 2016

UWAJIBIKAJI WA VIONGOZI KWA USTAWI BORA WA MWANANCHI.


BY NGUDU NYUMBANI BLOG
18/06/2016

Katika jitihada za kuona jamii yetu inapiga hatua moja zaidi mbele, na pengine kutoka hali iliyopo sasa kuna haja ya uwajibikaji mkubwa kwa viongozi na wananchi kwa ujumla.

Nilikuwa najaribu kupitia ripori ya mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) ya mwaka 2015, Kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za miradi ya mendeleo kwenye halmashauri zetu.
Hasa nikiangalia kwenye jamii yetu ya Kwimba, ripoti ni nzuri kidogo tofauti na ya miaka kadhaa iliyopita ambapo wilaya haikuwa na hati ya kuridhisha kwa maana ya kuwa na kasoro na mapungufu mengi katika kutekelza miradi ya maendeleo.

Katika miradi mitano ya maendeleo iliyokaguliwa na kutolewa ripoti, walau miradi minne imefanya vizuri kasoro mmoja ambao haujafanya vizuri. Programu ya maendeleo ya kilimo(ASDP), mfuko wa afya(HBF), mfuko wa barabara(RF) na Programu ya maendeleo ya sekta ya maji(WSDP) ndiyo iliyopata hati inayoridhisha, huku mfuko wa maendeleo ya jamii(TASAF) ukipata hati isiyoridhisha.

Pamoja na  baadhi ya miradi hiyo kufanya vizuri lakini ripori imetaja changamoto na mapungufu mbalimbali ambayo serikali inapaswa kutilia mkazo ili kuboresha miradi hiyo na mingine mingi inayofanyika katika jamii zetu.
Mfano mpango wa maendeleo wa kilimo wa wilaya(DADP), unashughulikia vipi changamoto anazokumbana nazo mkulima wa pamba, alizeti na mazao mengine anayolima mkulima wa Kwimba?. Vipi kuhusu kilimo cha umwagiliaji kwa baadhi ya maeneo kinapewa msisitizo gani katika kumkomboa mwananchi wa kawaida anayetegemea kilimo kujikimu na hali ya maisha.

Katika taarifa mbalimbali za serikali, Halmashauri zote nchini zimeshauriwa kutekeleza maazimio 12 yaliyoazimiwa na wakuu wa mikoa, mkoani Dodoma mwaka 2014 ili kuainisha changamoto za ukosefu wa ajira kwa vijana na utatuzi wake.

 Katika hili ushirikishwaji wa mwananchi ni muhimu sana ili halmashauri ziweze kubaini changamoto haswa zinazowakabili vijana wengi kwenye suala la ajira na namna bora ya kushughulika nazo, ikiwa ni pamoja na Mipango mathubuti ya kuwasaidia. Niliwahi kuandika huko nyuma nikimshauri diwani wangu kwa niaba ya madiwani wenngine suala la fursa za ujasiliamali.
Pia katika kusomasoma habari mbalimbali niliona habari ya halmashauri moja ambapo baraza la madiwani walipitisha mpango wa bima ya afya ulioboreshwa .unaotolewa na mfuko wa hifadhi za jamii CHF kwa kuwa umepanua wigo wa matibabu kwa wananchi wengi waishio vijijini na kurekebisha masharti ya kujiunga. 
Sina hakika kama kwetu tumefikia huku, kama na kwetu hali ipo hivi basi ni vizuri. Ila kama bado kuna haja ya viongozi tuliowachagua kuangalia uwezekano wa kupendekeza masuala ya muhimu kama haya kama njia mojawapo ya kuboresha ustawi wa wananchi wao.
Suala la watumishi hewa na mishahara hewa kwenye taasisi nyingi za serikali mathalan halmashauri kufikia sasa limefanyiwa kazi kwa ustadi mkubwa kiasi cha kuokoa fedha nyingi zilizokuwa zinatumiwa na watu wachache. Kia halmashauri ya wilaya ilikwa inawajibika kubaini watumishi hewa kupitia idara zote zilizo chini ya halmashauri hizo.

Zoezi hili linapaswa kuwa endelevu kwa maana ya kudhibiti ufujaji wa mali za umma. Na pia wahusika wote walioiingizia serikali hasara kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Kuanzia april na  mwezi may mwaka huu(2016) kuna mradi wa uimarishaji mifuko ya sekta za umma(PS3) ambapo katika mkoa wa mwanza umeanza na wilaya mbili za KWIMBA na SENGEREMA ambapo mradi huo utatekelezwa kwa miaka mitano katika awamu ya kwanza. mradi unafadhiliwa na shirika la maendeleo la kimataifa la marekani(USAID).
kwa kila mkoa zimetengwa wilaya mbili zenye mahitaji makubwa ya uboreshaji mifumo yake ya sekta za umma.
Matarajio makubwa ya mradi huu utaimarishwa katika ngazi ya kitaifa na katika halmashauri, ili kutumia rasilimali kwa uwazi, kwa kuwezesha ushirikishwaji wa wananchi katika kupanga na kufuatilia na kutoa matokeo ya ufanisi wa kazi kwa kila sekta.
maeneo ya utekelezaji wa mradi huo ni Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Raia, Rasilimali Watu, Rasilimali Fedha, Mifumo ya Mawasiliano na Utafiti Tendaji (Operational Research).

Katika hatua nyingine inashauliwa kwamba, kila hamashauri inapaswa kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajiri ya kuviwezesha vikundi mbalimbali vya ujasiriamali mathalan vinavyowahusu vijana na wanawake.  
Hili limekuwa likilalamikiwa kutofanyika kama inavyopaswa, ama kwa wakurugenzi au watendaji wa halmashauri kadhaa kutotenga kiwango hicho cha asilimia kwa kuviwezesha vikundi na kuvisimamia viweze kukidhi matakwa na mahitaji yao na ya jamii nzima kwa ujumla.

Aidha, halmashauri inapaswa kupanga bajeti yake ya miradi ya maendeleo inayopaswa kutekelezwa kabla ya bajeti ya serikali kupitia bajeti za wizara hazijapitishwa na bunge. Hilo limekwisha fanyika kwa halmashauri zote mpaka sasa, na baadhi kuweka wazi Mipango ya mabaraza yao ya madiwani kuhusu utekelezaji wa miradi yao waliyoiainisha katika bajeti zao. 
Sina hakika kama na kwetu wana utamaduni huo wa kuwafanya wananchi wao kujua nini kinapaswa kufanywa na kwa muda gani.

Nilijaribu kupitia mifumo ya bajeti za halmashauri na kuona mpangilio wa vyanzo vya mapato ya upangaji na uendeshaji wa bajeti hizo ambapo ni pamoja na;  Ruzuku kutoka Serikali Kuu; masharti, jumla & sawia; Mapato ya Ndani ya H/M; Fedha za Wahisani; Mikopo toka taasisi za kifedha, ikiwemo LGLB, Municipal Bounds; Michango ya wananchi,taasisi za hiari pamoja na nguvu kazi ya wananchi.

Kufanya kilicho sahihi kunahitaji zaidi muongozo wa maadili sahihi, ni imani viongozi tuliowachagua wakishirikiana na viongozi wandamizi wa serikali kufuata utaratibu sahihi wa kufanya kilich sahihi pia.
Katika kufanikisha hilo kuna mambo kadhaa ya kuzingatia. Moja, kuzingatia taaluma katika kutoa huduma bora na stahiki, pia kufanya kazi kwa bidii, kutokuwa na upendeleo na  kuwa na matumizi sahii ya taarifa za uendeshaji Mipango.

Pili, ni viongozi kuwa waaminifu kwa maana ya kufuata maadili ya kazi wanazozifanya. Na mwisho ni kutimiza wajibu wao. Katika kutimiza wajibu kunahitaji mambo kama utii kwa serikali, Kuwajibika kwa umma, pamoja na Kuheshimu na kutii sheria.

Bila kuzingatia mambo ya msingi kama hayo, ni dhahiri mambo yatakuwa sege mnege kwa sababu kila mtu anaweza kufanya awezalo ilimradi aonekane amefanya jambo.  Siku zote utekelezaji wa Mipango kwa kadri ilivyopaswa ni tiba mujarabu katika kuboresha maisha ya wananchi. uwajibikaji wa viongozi huchochea ustawi bora wa maendeleo ya mwananchi!

Tafakari!
NGUDU NYUMBANI BLOG
nguduone@gmail.com.



Previous Page Next Page Home