Sunday, January 24, 2016

MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE(SFNA) 2015


BY NGUDU NYUMBANI BLOG

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), limetangaza matokeo ya mitihani ya kujipima ya darasa la nne huku matokeo hayo yakionyesha wanafunzi wengi wamefeli katika somo la Kiingereza kwa asilimia 65.67 katika mitihani hiyo iliyofanyika mwishoni 2015.

Akitangaza matokeo hayo  Jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt. Charles Msonde amesema juhudi za makusudi zinahitajika katika kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzia ili kuboresha kiwango cha ufaulu.

Jumla ya wanafunzi 869,057 kati ya wanafunzi 977,886 sawa na asilimia 88.87 waliofanya upimaji wamepata alama katika madaraja ya A,B,C, na D. Wanafunzi 108,829 sawa na asilimia11.13 wamepata alama za ufaulu usioridhisha.

Aidha wanafunzi wamefanya vizuri zaidi katika somo la Sayansi kwa asilimia 89.44, na baraza limewataka walimu kuweka mkazo zaidi kwa wanafunzi waliofanya vibaya ili wawasaidie kuimarika na waweze kupata ufaulu mzuri.

MATOKEO UPANDE WA WILAYA YA KWIMBA

Kwa upande wa matokeo hayo ya upimaji wa kitaifa darasa la nne, ambapo kuna jumla ya shule za msingi 151.

Baadhi ya Shule za msingi zilizoongoza katika upimaji wa matokeo hayo ni kama ifuatavyo;

1. KINAMWELI PRIMARY SCHOOL

2. NG'WAMAKOYE PRIMARY SCHOOL

3. MWAKILYAMBITI PRIMARY SCHOOL

4. MWANG'HALANGA PRIMARY SCHOOL



Baadhi ya Shule zilizofanya vibaya katika upimaji huo ni;

149. NG'WANG'HANGA PRIMARY SCHOOL


151. NG'WAMAPALALA PRIMARY SCHOOL

Matokeo yote upande wa wilaya yetu ya Kwimba unaweza kuyapata kupitia link hii


>>>> MATOKEO

au ukiingia kwenye tovuti ya NECTA

No comments:

Post a Comment

Previous Page Next Page Home