HOTUBA YA
MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI
WA KUHITIMISHA SHUGHULI ZA MKUTANO
WA 18 WA
BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TAREHE 7
FEBRUARI, 2015
I:
UTANGULIZI
(a) Masuala ya jumla
1. Mheshimiwa Spika, Tumekuwepo hapa kwa takriban siku 12 katika
shughuli za Mkutano wa 18 wa Bunge lako Tukufu. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi
Mungu mwenye wingi wa Rehema kwa kutufikisha salama siku ya leo.
2. Lakini tumekutana hapa tukiwa tumeshuhudia mabadiliko katika Baraza la
Mawaziri na Wenyeviti wa baadhi ya Kamati za Kudumu za Bunge. Niruhusu nitumie
nafasi hii ya awali kuwapongeza Mawaziri na Naibu Mawaziri wote ambao
wameteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali katika mabadiliko hayo. Aidha, napenda
niwapongeze Wenyeviti watatu pamoja na Makamu mmoja kwa kuchaguliwa kuongoza Kamati
za Kudumu za Bunge ikiwemo Kamati ya Bajeti, Kamati ya Nishati na Madini na
Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala. Tunawatakia afya njema Mawaziri, Naibu
Mawaziri na Wenyeviti wote katika kutekeleza majukumu yao mapya.
3. Mheshimiwa Spika,Tangu tulipomaliza Mkutano wa 16 na 17 wa Bunge lako
Tukufu, kumetokea majanga katika sehemu mbalimbali Nchini ikiwemo mafuriko na
mapigano ya Wakulima na Wafugaji kule Morogoro, pamoja na ajali za barabarani.
Naomba nitumie nafasi hii kuwapa pole wote walioathirika na majanga, maafa na
ajali za barabarani. Kwa wale waliopoteza maisha tunawaombea kwa Mwenyezi
Mungu azilaze roho za marehemu mahala pema peponi Amina.
b)
Maswali
4. Mheshimiwa Spika, Katika Mkutano huu, Waheshimiwa Wabunge wamepata fursa ya kuuliza maswali
ya kawaida na yale ya papo papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Jumla ya maswali
122 ya msingi na 313 ya nyongeza yaliulizwa na Waheshimiwa Wabunge na kujibiwa
na Serikali. Aidha, Maswali 15 ya msingi na 13 ya nyongeza yaliulizwa na
kujibiwa kwa utaratibu wa maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.
(c) Miswada na Taarifa Mbalimbali
5. Mheshimiwa Spika, Tunahitimisha Mkutano huu tukiwa tumekamilisha kazi
kubwa ya kusoma na kujadili taarifa mbalimbli za Kamati za Bunge za Kisekta na
zisizo za Kisekta. Kamati za Kisekta ambazo Taarifa zake zimewasilishwa na
kujadiliwa na Waheshimiwa Wabunge ni zifuatazo:
i.
Kamati ya Miundombinu;
ii.
Kamati ya Nishati na Madini;
iii.
Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira;
iv.
Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji;
v.
Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala;
vi.
Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa;
vii.
Kamati ya Masuala ya UKIMWI;
viii.
Kamati ya Ulinzi na Usalama;
ix.
Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa;
x.
Kamati ya Huduma na Jamii; na
xi.
Kamati ya Maendeleo ya Jamii.
6. Aidha, Bunge Lako Tukufu
lilipokea na kujadili Taarifa za Kamati zisizo za Kisekta zinazosimamia Fedha
za Umma zifuatazo:
i.
Kamati ya Hesabu za Serikali;
ii.
Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa; na
iii.
Kamati za Bajeti.
No comments:
Post a Comment