Monday, February 9, 2015

SHIRIKA LA MAALBINO DUNIANI LAMSUTA MBUNGE WA KWIMBA

Mkurugenzi wa shirika la Under The Same Sun (UTSS), Peter Ash

SHIRIKA la Under The Same Sun (UTSS) limeeleza kusikitishwa kwake na viongozi wa kisiasa pamoja na mbunge wa jimbo la kwimba kutofika kumjulia hali na kumfariji mama wa motto mwenye ulemavu wa ngozi, Pendo Emmanuel (4) aliyeporwa na watu wasiojulikana mwishoni mwa mwaka jana.
Hayo yalielezwa jana na Mkurugenzi wa Mwanzilishi wa shirika hilo, Peter Ash wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara yake kwenye mikoa ya Mwanza na Shinyanga
“Nimefika kwenye kijiji cha Ndami wilayani Kwimba, motto pendo alipotekwa na kuzungumza na  wazazi wake ambaye alieleza kuwa mbunge wa jimbo hilo hajaenda kumtembelea ili kujua  motto wake yupo  wapi na anashangaa yeye kutoka Canada amefika”, alisema na kuongeza kwanini mbunge ambaye yeye anampigia kura hajaenda kumsikiliza.
Alisema January 6, mwaka huu katika eneo la Nyakato, motto mwingine mwenye ulemavu wa ngozi , karim kassimalinusurika kutekwa ambapo familia yake nayo inasema hakuna kiongozi wa siasa wala Mbunge walioenda kuwajulia hali.
Ash alisema watu wenye ulemavu wa ngozi wamekuwa wakiwindwa na wanaendelea kuwindwa hasa wakati huu kuelekea uchaguzi ambapo Tanzania na Burundi zinafanya uchaguzi mwaka huu na kuhoji kwa nini vitendo vya ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi vinazidi kuongezeka kipindi hiki.
Alisema kumekuwepo na matukio 152 yakiwemo ya utekaji nyara, kubakwa na mauaji ambayo yametokea kwa kipindi cha miaka 14 nchini Tanzania; lakini ni asilimia tano tu ya kesi ndio zimefikishwa mahakamani ambazo hazilingani na idadi ya matukio na watu waliofanyiwa ukatili.
Alisema viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi vinauzwa kwa bei juu, lakini cha kujiuliza ni nani atakuwa na maelfu ya dola ili kununua hivyo viungo isipokuwa wale watu ambao ni matajiri, Watanzania wengi ni masikini.
Mtoto Pendo Emmanuel (4) aliporwa na watu wasiojulikana December 27, mwaka jana wakati akiwa amelala na wazazi wake katika kijiji cha Ndami, tarafa ya Mwamashimba wilayani Kwimba, majira ya saa 4 usiku.


 Chanzo: Habari leo

No comments:

Post a Comment

Previous Page Next Page Home