Thursday, May 21, 2015

MTIA NIA MWINGINE JIMBO LA KWIMBA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MWAKA HUU



Heshima kwenu wakubwa,Mimi ni mtanzania mwenye akiri timamu {Aged 26 years old},bila kushurutishwa na mtu yeyote yule nimeamua kutangaza nia mapema kabisa ya kugombea ubunge jimbo la kwimba 2015.Nina degree ya falsafa na Elimu kutoka chuo kikuu cha mtakatifu Agustino Mwanza {SAUT}.Bachelor of philosophy with education.Nimetarajia kufanya mambo yafuatayo.

1. Kununua magari mawili kwa kutumia hera za mfuko wa jimbo ndani ya miaka miwili,Gari moja litabaki ngudu mjini na lingine litakuwa Mwamashimba.Kazi ya magari haya ni kama ifuatavyo:

A-   Kupeleka wagonjwa hospitarini wanaotoka vijiji vya mbali kama vile,Mahiga,Nyamilama,Bugembe, Mwang'haranga,shilaboya,mwadub i,jojiro pamoja na maeneo mengine.Vile vile na gari litakalokuwa Mwamashimba nalo litafanya kazi vilevile.

B-   Kusomba mchanga na mawe pamoja na shughuri zingine ili kutengeneza mfuko kwa ajiri ya kusomesha watoto yatima.

2. Kufanya mkakati wa kutengeneza barabara ya kutoka ngudu mjini kupitia jojiro hadi mabuki kwa kiwango cha lami,barabara ya kutoka mjini kupitia sumve hadi Magu kwa kiwango cha lami,barabara ya kutoka ngudu mjini kupitia mahiga,Nyamilama hadi Hungumalwa kwa kiwango cha lami.Nitashirikiana na atakaye kuwa mbunge wa maswa kufanya mpango wa kuitengeneza barabara ya kutoka Maswa kupitia,Shigumhulo,jojiro hadi mwabuki kwa kiwango cha Lami.

3.  Kufanya mkakati wa kuweka umeme kwenye center zote ambazo zitapitiwa na barabara ya lami kama vile Nyamilama,Lunele,Jojiro,Mwamas himba na maeneo mengine.
3.Kushugurikia suala la maji.Ni mengi sana ila naomba niishie hapo.

UFISADI ULIOFANYWA NA MBUNGE WA SASA WA KWIMBA (KAKA MANSOURI-CCM)

1.Kutumia hera ya mfuko wa jimbo milioni mia mbili na laki moja kwenye miladi yake.
2.Kuhamisha miladi ya barabara mbili za wilaya ya kwimba kwenda Bariadi zilizopaswa kutengenezwa kwa kiwago cha lami.
Haya ni machache tu,mengi yanakuja.

Ndugu wana wa Kwimba na watanzania kwa ujumla popote pale mlipo wenye mapenzi ya dhati kabisa na nchi yetu na mnaochukizwa na matumizi mambaya ya Raslimali zetu,pasipo kubagua dini pamoja na vyama nahitaji sana mchango wenu wa khari na mali ili niweze kufikia malengo yangu ya kuondoa matatizo ya jimbo la kwimba na Tanzania kwa ujumla.Kwa haya yote namtanguliza mwenyezi mungu katika Malengo yangu.Nasema hivi kwa sababu gani,umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.Napenda sana changamoto pamoja na ushauri.

JINA.MARTIN WILBERT MANDAGO PHILLPO.
MAHARI.ILAMBA NGUDU-KWIMBA
UMRI - MIAKA 26
KABILA. MSUKUMA
CONTACT.PHONE NO.0765183733


No comments:

Post a Comment

Previous Page Next Page Home