Saturday, April 9, 2016

WATU NINAOJIVUNIA KATIKA TASNIA YA SANAA KWIMBA KWETU (SEHEMU YA PILI)


BY NGUDU NYUMBANI BLOG
09/04/2016

 Huu ni mwendelezo wa makala iliyopita juu ya kukubali na kupenda vipaji vya watu hususan kwenye tasnia Sanaa. Ikiwa wengi wao walifanya na baadae wakaacha, ila wengine wanajihusisha na mambo hayo hadi leo.

Lengo kubwa na la msingi katika kuyajua haya yote, ni kutaka kuiandika historia ya wilaya yetu iweze kukumbukwa na wengi japo pengine isiwe imekamilika kwa asilimia zote.
Kipindi cha nyuma kuliwahi kuwapo na kundi la HIP HOP lililojulikana kwa jina la MASOKWE FAMILY liliundwa na vichwa vitatu  likiongozwa Mwl. Wawa a.k.a CRAZY V.
Kwa sasa Wawa ni mwalimu anayefundisha watoto wenye special needs kakora s/m.

Pia kulikuwa na kundi la muziki la BLESSED BOYS baadae likabadilishwa na kuwa BLESSED ARMY.  kundi hili liliundwa na Renatus Mahuyu(ray m), Deogratias Igonzela(yung skills), Samwel Musobi(samu 4 real), Yahya (yq), Shaina(lady shao), Zephania festo(zf), pia kulikia na dogo felali. Kwa sasa wengi wao kama sio wote ni waheshimiwa kulingana na nafasi walizonazo.
 Na pengine ukiwakumbusha wakupe stori kidogo juu ya harakati zao enzi hizo, vijana wa mjini wanasema ‘ilikuwa ni shiida’ enzi hizo.

Ukiachilia mbali makundi ya muziki, naambiwa pia FRED  SWAGG ni KWIMBA product. Huyu jamaa anajulikana sana hasa kwa wafuatiliaji wazuri wa muziki wetu. Amewahi kufanya ngoma kama  THE LYRICS akiwashirikisha Young killer(msodoki) na Kad go(kadi ya mchezo). Pia nyingine akimshirikisha Baraka Da prince kwenye track ya ‘Kikomo’, na nyingine nyingi.

Unaweza kuona muziki hasa wa Hip Hop uliweza kuvutia vijana wengi sana, hata leo bado unavutia wengi pia. Zamani kulikuwa na changamoto nyingi tofauti na sasa katika kuufanya. Muziki huu umeendelea kutambulika kama muziki wa harakati ambapo kwa wafuatiliaji wazuri wanajua kuna Misingi na Nguzo zinazoongoza mziki huu.

Ukiachana na hilo, harakati za kuukuza mziki huu ni nyingi, ambapo kumekuwepo na vitu kama KILINGE CHA NADHALIA kwa wakazi wa Dar(New msasani club chini ya usimamizi wa tamaduni muzik), S.U.A kwa wakazi wa Arusha(kijenge juu, chini ya watengwa rec) kama waanzilishi ambapo kwa sasa ni karibu kila mkoa kuna haya mambo. Pia kwa Mwanza kuna S.U.A  maeneo ya nyamagana.

Dj Venture, ni moja ya watu muhimu kabisa kipindi hicho miaka ya 2002 hivi. Ikumbukwe ndiye aliyefanikisha kuwaleta wasanii wengi wakubwa  Bob Haisa, Inspecta Haroun na wengine wengi ambao baadhi niliwaongelea kwenye sehemu ya kwanza ya makala hii.
Mbali na kufanikisha kwa kiasi kikubwa kuleta wasanii kufanya show wilayani, pia anaongelewa kufanikisha kwa kiasi kikubwa kuletwa na kuanzishwa kwa MISS KWIMBA.

Katika kufanikisha hilo kulikuwa na kamati maalumu ya kupanga na kufanikisha tukio hilo. Ambapo inasemekana waliounda kamati hiyo ni pamoja na Dj jigga, Idd ghati, Daniel Magobe, Mbialo na wengineo.

Baada ya muda, tukio la Miss KWIMBA  lilizoeleka na kupata wafuasi na washiriki wengi pia. Itakumbukwa hadi watoto wa sekondari walihusika hapo. Ndiyo kipindi cha kina NYABAZENDA MATENGANE kuwatoa kimasomaso vijana wa NGOYAI pale Ngudu sec, pale aliponyakua taji hilo.

Pia katika ma-DJ vijana wanaochipukia na kukubalika vema  nilisahau jina la bwana mdogo Nestory Samson. Ni moja ya vijana mahiri kabisa katika eneo hilo la kuchezea vyombo vya muziki.

Kwenye sanaa, upande wa wachoraji na wapaka rangi bora kabisa enzi hizo pengine hadi leo. Utakutana na Mwenyekiti wa sasa wa NGUDU MJINI, mh Casmiry Antony, bila kumsahau J4 kama tulivyomjua wengi.

WASANII WASUKUMA(nyimbo za asili)

Katika kanda ya ziwa, hasa sehemu ambazo zinakaliwa na kabila la wasukuma nikihusisha na eneo letu pia. Kumekuwepo na mwamko mkubwa wa wasanii wa nyimbo za asili hasa nikimaanisha nyimbo za kisukuma.

Kuna wasanii wengi ambao wanafanya vizuri katika anga hiyo kama, Bhulemela, Bhudagala, Senghi milembe, Inaga Myambelele, Juma Marko, Kundi wa Moto, Madebe, Steven Maneno, Misoji sabhujo, Nyanda Lunduma, Kisima, Koper head, Elias mnyamwezi, Mwana kwela, Shinje makala, Mchelemchele, Jeledi, Malingita, Shilango na wengine wengi.
Utajiuliza nimewajuaje wote hao, ila ukweli ni kwamba nimewafahamu kupitia nyimbo zao nilizonazo. Japo mimi nae ni mmoja kati ya wavivu wengi wa kusikiliza ladha adhimu hii kutoka usukumani. Na katika wote niliowataja hapo juu sina hakika kama kuna hata mmoja anatokea KWIMBA kwetu. Katika kundi kama hilo, pia kuna wacheza ngoma maarufu ambapo wamekuwa wakifanya mashindano mara kadhaa hasa viwanja vya KWIDECO na MAHIGA na maeneo mengine ndani na nje ya wilaya.

‘Kila ng’wene na ka nyengele gakwe’, moja ya misemo maarufu ya kisukuma. Ikilenga kumaanisha kila mmoja kwa nafasi yake katika kutoka au kufanya kitu.  Panapo majaliwa WAKATABAHU.

KWIMBA TUITAKAYO
nguduone@gmail.com



1 comment:

  1. N kwel muzk wetu bado sana japo kuna jthada za hapa na pale ila nan tunaweza tatzo n wawezeshaj ndo shda pia hatuna hata steshen ya radio kwa ajr ya promo za nymbo pia hatuna hata studio moja ya kurecod audio ..naamn kufkia baada ya miaka miwl lazma mzk wetu ubadrke ktk maboresho zaid ya kimafankio, Mungu ibark ngudu ktk Sana'a ya mzk

    ReplyDelete

Previous Page Next Page Home